Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 31:11-23 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Mumewe humwamini kwa moyo,kwake atapata faida daima.

12. Kamwe hamtendei mumewe mabaya,bali humtendea mema maisha yake yote.

13. Hutafuta sufu na kitani,na kufanya kazi kwa mikono yake kwa bidii.

14. Yeye ni kama meli za biashara:Huleta chakula chake kutoka mbali.

15. Huamka kabla ya mapambazuko,akaitayarishia jamaa yake chakula,na kuwagawia kazi watumishi wake.

16. Hufikiria kununua shamba, kisha hulinunua,na kulima zabibu kwa faida ya jasho lake.

17. Huwa tayari kufanya kazi kwa nguvuna kuiimarisha mikono yake.

18. Hutambua kwamba shughuli zake zina faida;hufanya kazi hata usiku kwa mwanga wa taa yake.

19. Husokota nyuzi kwa mikono yake mwenyewe,kwa vidole vyake mwenyewe husuka nguo zake.

20. Huufungua mkono wake kuwapa maskini,hunyosha mkono kuwasaidia fukara.

21. Hawahofii watu wake ijapo baridi ya kipupwe,maana kila mmoja anazo nguo za kutosha.

22. Hujitengenezea matandiko,mavazi yake ni ya zambarau ya kitani safi.

23. Mume wake ni mtu mashuhuri barazani,anakoshiriki vikao vya wazee wa nchi.

Kusoma sura kamili Methali 31