Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 31:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Maneno ya mfalme Lemueli. Mawaidha aliyofundishwa na mama yake:

2. Nikuambie nini mwanangu?Nikuambie nini mwanangu niliyekuzaa?Nikuambie nini wewe niliyekuomba kwa Mungu?

3. Usimalize nguvu zako kwa wanawake,usiwape mali yako hao wanaoangamiza wafalme.

4. Haifai ee Lemueli, haifai wafalme kunywa divai,wala wakuu kutamani vileo.

5. Wakinywa watasahau maagizo ya sheria,na kuwanyima haki wenye taabu.

Kusoma sura kamili Methali 31