1. Maneno ya mfalme Lemueli. Mawaidha aliyofundishwa na mama yake:
2. Nikuambie nini mwanangu?Nikuambie nini mwanangu niliyekuzaa?Nikuambie nini wewe niliyekuomba kwa Mungu?
3. Usimalize nguvu zako kwa wanawake,usiwape mali yako hao wanaoangamiza wafalme.
4. Haifai ee Lemueli, haifai wafalme kunywa divai,wala wakuu kutamani vileo.
5. Wakinywa watasahau maagizo ya sheria,na kuwanyima haki wenye taabu.