Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 3:29-35 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Usipange maovu dhidi ya jirani yako,anayeishi karibu nawe bila wasiwasi.

30. Usigombane na mtu bila sababuikiwa hajakudhuru kwa lolote.

31. Usimwonee wivu mtu mkatili,wala usiige mwenendo wake.

32. Maana waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu;lakini yeye huwafanya marafiki zake wale walio wanyofu.

33. Mwenyezi-Mungu huapiza nyumba za waovu,lakini huyabariki makao ya waadilifu.

34. Yeye huwadharau wenye dharau,lakini huwafadhili wanyenyekevu.

35. Wenye hekima watavuna heshima,lakini wapumbavu watapata fedheha.

Kusoma sura kamili Methali 3