Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 3:21-34 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Mwanangu, zingatia hekima safi na busara;usiviache vitoweke machoni pako,

22. navyo vitakuwa uhai nafsini mwako,na pambo zuri shingoni mwako.

23. Hapo utaweza kwenda zako kwa usalama,wala mguu wako hautajikwaa.

24. Ukiketi hutakuwa na hofu;ukilala utapata usingizi mtamu.

25. Usiogope juu ya tishio la ghafla,wala shambulio kutoka kwa waovu,

26. Maana Mwenyezi-Mungu ndiye atakayekutegemeza;atakuepusha usije ukanaswa mtegoni.

27. Usimnyime mtu anayehitaji msaada,ikiwa unao uwezo wa kufanya hivyo.

28. Usimwambie jirani yako aende zake hadi kesho,hali wewe waweza kumpa anachohitaji leo.

29. Usipange maovu dhidi ya jirani yako,anayeishi karibu nawe bila wasiwasi.

30. Usigombane na mtu bila sababuikiwa hajakudhuru kwa lolote.

31. Usimwonee wivu mtu mkatili,wala usiige mwenendo wake.

32. Maana waovu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu;lakini yeye huwafanya marafiki zake wale walio wanyofu.

33. Mwenyezi-Mungu huapiza nyumba za waovu,lakini huyabariki makao ya waadilifu.

34. Yeye huwadharau wenye dharau,lakini huwafadhili wanyenyekevu.

Kusoma sura kamili Methali 3