18. Hekima ni mti wa uhai kwa wote wampatao;wana heri wote wanaoshikamana naye.
19. Kwa hekima Mwenyezi-Mungu aliweka misingi ya dunia,kwa akili aliziimarisha mbingu.
20. Kwa maarifa yake vilindi vilipasuka,na mawingu yakadondosha umande.
21. Mwanangu, zingatia hekima safi na busara;usiviache vitoweke machoni pako,
22. navyo vitakuwa uhai nafsini mwako,na pambo zuri shingoni mwako.
23. Hapo utaweza kwenda zako kwa usalama,wala mguu wako hautajikwaa.
24. Ukiketi hutakuwa na hofu;ukilala utapata usingizi mtamu.