Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 3:16-21 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Kwa mkono wake wa kulia Hekima atakupa maisha marefu;kwa mkono wake wa kushoto atakupa mali na heshima.

17. Njia zake ni za kupendeza,zote zaelekea kwenye amani.

18. Hekima ni mti wa uhai kwa wote wampatao;wana heri wote wanaoshikamana naye.

19. Kwa hekima Mwenyezi-Mungu aliweka misingi ya dunia,kwa akili aliziimarisha mbingu.

20. Kwa maarifa yake vilindi vilipasuka,na mawingu yakadondosha umande.

21. Mwanangu, zingatia hekima safi na busara;usiviache vitoweke machoni pako,

Kusoma sura kamili Methali 3