15. Hekima ina thamani kuliko johari,hamna unachotamani kiwezacho kulingana nayo.
16. Kwa mkono wake wa kulia Hekima atakupa maisha marefu;kwa mkono wake wa kushoto atakupa mali na heshima.
17. Njia zake ni za kupendeza,zote zaelekea kwenye amani.
18. Hekima ni mti wa uhai kwa wote wampatao;wana heri wote wanaoshikamana naye.
19. Kwa hekima Mwenyezi-Mungu aliweka misingi ya dunia,kwa akili aliziimarisha mbingu.
20. Kwa maarifa yake vilindi vilipasuka,na mawingu yakadondosha umande.
21. Mwanangu, zingatia hekima safi na busara;usiviache vitoweke machoni pako,
22. navyo vitakuwa uhai nafsini mwako,na pambo zuri shingoni mwako.
23. Hapo utaweza kwenda zako kwa usalama,wala mguu wako hautajikwaa.
24. Ukiketi hutakuwa na hofu;ukilala utapata usingizi mtamu.
25. Usiogope juu ya tishio la ghafla,wala shambulio kutoka kwa waovu,
26. Maana Mwenyezi-Mungu ndiye atakayekutegemeza;atakuepusha usije ukanaswa mtegoni.