Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 3:11-24 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Mwanangu, usidharau adhabu ya Mwenyezi-Mungu,wala usiudhike kwa maonyo yake;

12. maana Mwenyezi-Mungu humwonya yule ampendaye,kama baba amwonyavyo mwanawe mpenzi.

13. Heri mtu anayegundua hekima,mtu yule anayepata ufahamu.

14. Hekima ni bora kuliko fedha,ina faida kuliko dhahabu.

15. Hekima ina thamani kuliko johari,hamna unachotamani kiwezacho kulingana nayo.

16. Kwa mkono wake wa kulia Hekima atakupa maisha marefu;kwa mkono wake wa kushoto atakupa mali na heshima.

17. Njia zake ni za kupendeza,zote zaelekea kwenye amani.

18. Hekima ni mti wa uhai kwa wote wampatao;wana heri wote wanaoshikamana naye.

19. Kwa hekima Mwenyezi-Mungu aliweka misingi ya dunia,kwa akili aliziimarisha mbingu.

20. Kwa maarifa yake vilindi vilipasuka,na mawingu yakadondosha umande.

21. Mwanangu, zingatia hekima safi na busara;usiviache vitoweke machoni pako,

22. navyo vitakuwa uhai nafsini mwako,na pambo zuri shingoni mwako.

23. Hapo utaweza kwenda zako kwa usalama,wala mguu wako hautajikwaa.

24. Ukiketi hutakuwa na hofu;ukilala utapata usingizi mtamu.

Kusoma sura kamili Methali 3