Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 3:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwanangu, usiyasahau mafundisho yangu,bali kwa moyo wako uzishike amri zangu.

2. Maana yatakupa wingi wa siku,maisha marefu na fanaka kwa wingi.

3. Utii na uaminifu visitengane nawe.Vifunge shingoni mwako;viandike moyoni mwako.

4. Hivyo utakubalika na kusifika,mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu.

5. Mtumaini Mwenyezi-Mungu kwa moyo wako wote,wala usitegemee akili zako mwenyewe.

6. Umtambue Mungu katika kila ufanyalo,naye atazinyosha njia zako.

7. Usijione wewe mwenyewe kuwa mwenye hekima;mche Mwenyezi-Mungu na kujiepusha na uovu.

8. Hiyo itakuwa dawa mwilini mwako,na kiburudisho mifupani mwako.

9. Mheshimu Mwenyezi-Mungu kwa mali yako,na kwa malimbuko ya mazao yako yote.

10. Hapo ghala zako zitajaa nafaka,na mapipa yako yatafurika divai mpya.

Kusoma sura kamili Methali 3