Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 29:2-8 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Waadilifu wakitawala watu hufurahi,lakini waovu wakitawala watu hulalamika.

3. Apendaye hekima humfurahisha baba yake;lakini aandamanaye na malaya hufuja mali yake.

4. Mfalme akitumia haki huipatia nchi uthabiti,lakini akipenda hongo taifa huangamia.

5. Mwenye kumbembeleza jirani yake,anatega mtego wa kujinasa mwenyewe.

6. Mtu mbaya hunaswa kwa kosa lake,lakini mtu mwadilifu huimba na kufurahi.

7. Mwadilifu anajua haki za maskini,lakini mtu mwovu hajui mambo hayo.

8. Wenye dharau huutia vurugu mji mzima,lakini wenye hekima hutuliza ghadhabu.

Kusoma sura kamili Methali 29