Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 29:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Anayeonywa mara nyingi akawa mkaidi,ataangamia ghafla asipone tena.

2. Waadilifu wakitawala watu hufurahi,lakini waovu wakitawala watu hulalamika.

3. Apendaye hekima humfurahisha baba yake;lakini aandamanaye na malaya hufuja mali yake.

4. Mfalme akitumia haki huipatia nchi uthabiti,lakini akipenda hongo taifa huangamia.

5. Mwenye kumbembeleza jirani yake,anatega mtego wa kujinasa mwenyewe.

Kusoma sura kamili Methali 29