Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 29:1-15 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Anayeonywa mara nyingi akawa mkaidi,ataangamia ghafla asipone tena.

2. Waadilifu wakitawala watu hufurahi,lakini waovu wakitawala watu hulalamika.

3. Apendaye hekima humfurahisha baba yake;lakini aandamanaye na malaya hufuja mali yake.

4. Mfalme akitumia haki huipatia nchi uthabiti,lakini akipenda hongo taifa huangamia.

5. Mwenye kumbembeleza jirani yake,anatega mtego wa kujinasa mwenyewe.

6. Mtu mbaya hunaswa kwa kosa lake,lakini mtu mwadilifu huimba na kufurahi.

7. Mwadilifu anajua haki za maskini,lakini mtu mwovu hajui mambo hayo.

8. Wenye dharau huutia vurugu mji mzima,lakini wenye hekima hutuliza ghadhabu.

9. Mwenye hekima akibishana na mpumbavu,mpumbavu huwaka hasira na kucheka bila kutulia.

10. Wapendao kumwaga damu humchukia mtu asiye na hatia,lakini watu wema huyalinda maisha yake.

11. Mpumbavu huonesha hasira yake wazi,lakini mwenye hekima huizuia na kuituliza.

12. Mtawala akisikiliza mambo ya uongo,maofisa wake wote watakuwa waovu.

13. Maskini na mkandamizaji wanafanana kwa kitu kimoja:Wote wawili wamepewa macho na Mwenyezi-Mungu.

14. Mfalme anayewaamua maskini kwa haki,atauona utawala wake umeimarika milele.

15. Adhabu na maonyo huleta hekima,lakini mtoto aliyeachwa afanye apendavyo humwaibisha mama yake.

Kusoma sura kamili Methali 29