Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 28:8-18 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Aongezaye mali yake kwa riba na kutoza faidaanamkusanyia mwingine mwenye kuwahurumia maskini.

9. Anayekataa kuisikia sheria,huyo hata sala yake ni chukizo kwa Mungu.

10. Anayemshawishi mtu mwema kutenda mabaya,ataanguka katika shimo lake mwenyewe.Wasio na hatia wamewekewa mema yao.

11. Tajiri hujiona mwenyewe kuwa mwenye hekima,lakini maskini mwenye busara atamfichua.

12. Watu wema wakipata madaraka maisha hufana,lakini waovu wakitawala watu hujificha.

13. Afichaye makosa yake hatafanikiwa;lakini anayeungama na kuyaacha atapata rehema.

14. Heri mtu amchaye Mwenyezi-Mungu daima;lakini mkaidi wa moyo ataangukia maafa.

15. Mtawala mwovu anayewatawala maskini,ni kama simba angurumaye au dubu anayeshambulia.

16. Mtawala asiye na akili ni mdhalimu mkatili;lakini achukiaye mali ya udanganyifu atatawala muda mrefu.

17. Mtu anayelemewa na hatia ya kuua mtu,atakuwa mkimbizi mpaka kaburini;mtu yeyote na asijaribu kumzuia.

18. Aishiye kwa unyofu atasalimishwa,lakini mdanganyifu ataanguka kabisa.

Kusoma sura kamili Methali 28