Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 28:20-28 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Mtu mwaminifu atapata baraka tele,lakini mwenye pupa ya kuwa tajiri hataepa adhabu.

21. Si vizuri kumbagua mtu;watu hufanya mabaya hata kwa kipande cha mkate.

22. Mtu bahili hukimbilia mali,wala hajui kwamba ufukara utamjia.

23. Amwonyaye mwenzake hatimaye hupata mema zaidi,kuliko yule anayembembeleza kwa maneno matamu.

24. Anayeiba mali ya baba yake au mama yake, akasema si kosa,hana tofauti yoyote na wezi wengine.

25. Mchoyo huchochea ugomvi,lakini anayemtegemea Mwenyezi-Mungu atafanikiwa.

26. Anayetegemea akili yake mwenyewe ni mpumbavu;lakini anayeishi kwa hekima atakuwa salama.

27. Aliye mkarimu kwa maskini hatatindikiwa kitu,lakini anayekataa kuwaangalia atalaaniwa kwa wingi.

28. Waovu wakitawala watu hujificha,lakini wakiangamia, waadilifu huongezeka.

Kusoma sura kamili Methali 28