Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 28:13-24 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Afichaye makosa yake hatafanikiwa;lakini anayeungama na kuyaacha atapata rehema.

14. Heri mtu amchaye Mwenyezi-Mungu daima;lakini mkaidi wa moyo ataangukia maafa.

15. Mtawala mwovu anayewatawala maskini,ni kama simba angurumaye au dubu anayeshambulia.

16. Mtawala asiye na akili ni mdhalimu mkatili;lakini achukiaye mali ya udanganyifu atatawala muda mrefu.

17. Mtu anayelemewa na hatia ya kuua mtu,atakuwa mkimbizi mpaka kaburini;mtu yeyote na asijaribu kumzuia.

18. Aishiye kwa unyofu atasalimishwa,lakini mdanganyifu ataanguka kabisa.

19. Anayelima shamba lake atapata chakula kingi,bali anayefuata yasiyofaa atapata umaskini tele.

20. Mtu mwaminifu atapata baraka tele,lakini mwenye pupa ya kuwa tajiri hataepa adhabu.

21. Si vizuri kumbagua mtu;watu hufanya mabaya hata kwa kipande cha mkate.

22. Mtu bahili hukimbilia mali,wala hajui kwamba ufukara utamjia.

23. Amwonyaye mwenzake hatimaye hupata mema zaidi,kuliko yule anayembembeleza kwa maneno matamu.

24. Anayeiba mali ya baba yake au mama yake, akasema si kosa,hana tofauti yoyote na wezi wengine.

Kusoma sura kamili Methali 28