Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 26:18-27 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Kama mwendawazimu achezeavyo mienge,au mishale ya kifo,

19. ndivyo alivyo mtu ampotoshaye jirani,kisha aseme, “Nilikuwa natania tu!”

20. Bila kuni, moto huzimika;bila mchochezi, ugomvi humalizika.

21. Kama vile makaa au kuni huchochea moto,ndivyo mgomvi achocheavyo ugomvi.

22. Maneno ya msengenyaji ni kama kitoweo;hushuka mpaka ndani kabisa tumboni.

23. Kama rangi angavu iliyopakwa kigae,ndivyo yalivyo maneno matamu yenye nia mbaya.

24. Mwenye chuki huficha chuki yake kwa maneno mazuri,lakini huwa ana hila moyoni mwake.

25. Akiongea vizuri usimwamini,moyoni mwake mna chuki chungu nzima.

26. Huenda akaficha chuki yake,lakini nia zake mbaya zitajulikana kwa wote.

27. Amchimbiaye mwenzake shimo, hutumbukia mwenyewe;abingirishaye jiwe litamrudia mwenyewe.

Kusoma sura kamili Methali 26