Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 26:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Heshima apewayo mpumbavu haimfai;ni kama theluji ya kiangazi,au mvua ya wakati wa mavuno.

2. Kama shomoro au mbayuwayu wasiotua,kadhalika laana asiyostahili mtu haimtui.

3. Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda,na fimbo kwa mgongo wa mpumbavu.

4. Usimjibu mpumbavu kipumbavu,usije ukafanana naye.

5. Mjibu mpumbavu kama ustahilivyo upumbavu wake,asije akajiona kuwa mwenye hekima zaidi.

6. Kumtuma mpumbavu ujumbe,ni kama kujikata miguu au kujitafutia shida.

7. Methali mdomoni mwa mpumbavu,ni kama miguu ya kiwete inayoninginia.

8. Kumpa mpumbavu heshima,ni kama kufunga jiwe kwenye kombeo.

9. Mpumbavu anayejaribu kutumia methali,ni kama mlevi anayejaribu kungoa mwiba mkononi.

10. Mtu amwajiriye mpumbavu au mlevi,ni kama mpiga upinde anayejeruhi kila mtu.

Kusoma sura kamili Methali 26