Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 24:8-19 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Afikiriaye kutenda maovu daimaataitwa mtu mwenye fitina.

9. Mpango anaofikiria mpumbavu ni dhambi;mwenye dharau huchukiwa na kila mtu.

10. Ukifa moyo wakati wa shida,basi wewe ni dhaifu kweli.

11. Mwokoe mtu anayechukuliwa kuuawa bure;usisite kumwokoa anayeuawa bila hatia.

12. Usiseme baadaye: “Hatukujua!”Maana Mungu apimaye mioyo ya watu huona;yeye atakulipa kulingana na matendo yako!

13. Mwanangu, ule asali maana ni nzuri;sega la asali ni tamu mdomoni.

14. Ndivyo ilivyo hekima nafsini mwako;ukiipata utakuwa na matazamio mema,wala tumaini lako halitakuwa la bure.

15. Usivizie kama mwovu kushambulia makao ya mtu mwema,wala usijaribu kuiharibu nyumba yake,

16. maana mtu mwema huanguka mara nyingi lakini huinuka,lakini mtu mwovu huangamizwa na janga.

17. Usishangilie kuanguka kwa adui yako;usifurahie moyoni mwako kujikwaa kwake,

18. maana Mwenyezi-Mungu aonaye hayo hatapendezwa;huenda akaacha kumwadhibu.

19. Usihangaike kwa sababu ya watenda mabaya,wala usiwaonee wivu watu waovu,

Kusoma sura kamili Methali 24