Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 24:16-27 Biblia Habari Njema (BHN)

16. maana mtu mwema huanguka mara nyingi lakini huinuka,lakini mtu mwovu huangamizwa na janga.

17. Usishangilie kuanguka kwa adui yako;usifurahie moyoni mwako kujikwaa kwake,

18. maana Mwenyezi-Mungu aonaye hayo hatapendezwa;huenda akaacha kumwadhibu.

19. Usihangaike kwa sababu ya watenda mabaya,wala usiwaonee wivu watu waovu,

20. maana mwovu hatakuwa na mema baadaye;taa ya uhai wake itazimwa.

21. Mwanangu, umche Mwenyezi-Mungu na kumheshimu mfalme,wala usishirikiane na wale wasio na msimamo,

22. maana maangamizi yao huwapata ghafla.Hakuna ajuaye maafa watakayozusha.

23. Ifuatayo pia ni misemo ya wenye hekima:Kupendelea watu katika hukumu si vizuri.

24. Anayemwachilia mtu mwenye hatia,hulaaniwa na watu na kuchukiwa na mataifa.

25. Lakini wanaowaadhibu waovu watapata furaha,na baraka njema zitawajia.

26. Jibu lililo la haki,ni kama busu la rafiki.

27. Kwanza fanya kazi zako nje,tayarisha kila kitu shambani,kisha jenga nyumba yako.

Kusoma sura kamili Methali 24