Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 21:8-19 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Njia ya mtu mwenye hatia imepotoka,lakini mwenendo wa mnyofu umenyooka.

9. Afadhali kuishi pembeni juu ya paa,kuliko kuishi nyumbani na mwanamke mgomvi.

10. Anachopania kutenda mtu mbaya ni uovu;hata kwa jirani yake hana huruma.

11. Ukimwadhibu mwenye dhihaka, mjinga hupata hekima;ukimfundisha mwenye hekima, unampatia maarifa.

12. Mungu Mwadilifu anajua wanayotenda waovu nyumbani kwao;naye atawaangusha na kuwaangamiza.

13. Anayekataa kusikiliza kilio cha maskini,naye pia hatasikilizwa atakapolilia msaada.

14. Hasira hutulizwa kwa zawadi ya siri;tunu apewayo mtu imefichwa hupooza ghadhabu.

15. Haki ikitekelezwa watu wema hufurahi,lakini watu waovu hufadhaishwa.

16. Anayetangatanga mbali na njia ya busara,atajikuta ametua miongoni mwa wafu.

17. Anayependa anasa atakuwa maskini;anayefikiria tu kula na kunywa hatatajirika.

18. Mwovu atapata pigo ambalo halitampata mtu mwema,mkosefu ataadhibiwa badala ya mnyofu.

19. Afadhali kuishi jangwani,kuliko kukaa na mwanamke mgomvi na msumbufu.

Kusoma sura kamili Methali 21