Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 21:18-23 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Mwovu atapata pigo ambalo halitampata mtu mwema,mkosefu ataadhibiwa badala ya mnyofu.

19. Afadhali kuishi jangwani,kuliko kukaa na mwanamke mgomvi na msumbufu.

20. Nyumbani kwa mwenye busara mna hazina za thamani,lakini mpumbavu huponda mali yake yote.

21. Anayepania uadilifu na huruma,ataishi maisha marefu na kuheshimiwa.

22. Mwenye hekima aweza kuteka mji wa wenye nguvu,na kuziporomosha ngome wanazozitegemea.

23. Achungaye mdomo wake na ulimi wake,hujiepusha na matatizo.

Kusoma sura kamili Methali 21