Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 21:12-19 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Mungu Mwadilifu anajua wanayotenda waovu nyumbani kwao;naye atawaangusha na kuwaangamiza.

13. Anayekataa kusikiliza kilio cha maskini,naye pia hatasikilizwa atakapolilia msaada.

14. Hasira hutulizwa kwa zawadi ya siri;tunu apewayo mtu imefichwa hupooza ghadhabu.

15. Haki ikitekelezwa watu wema hufurahi,lakini watu waovu hufadhaishwa.

16. Anayetangatanga mbali na njia ya busara,atajikuta ametua miongoni mwa wafu.

17. Anayependa anasa atakuwa maskini;anayefikiria tu kula na kunywa hatatajirika.

18. Mwovu atapata pigo ambalo halitampata mtu mwema,mkosefu ataadhibiwa badala ya mnyofu.

19. Afadhali kuishi jangwani,kuliko kukaa na mwanamke mgomvi na msumbufu.

Kusoma sura kamili Methali 21