3. Ni jambo la heshima kuepa ugomvi;wapumbavu ndio wanaogombana.
4. Mvivu halimi wakati wa kulima;wakati wa mavuno atatafuta asipate chochote.
5. Fikira za mtu zimefichika kama kilindi cha maji;lakini mtu mwenye busara ajua kuzichota humo.
6. Watu wengi hujivunia kuwa wema,lakini mwaminifu wa kweli apatikana wapi?
7. Mtu mwadilifu akiishi kwa unyofu;watoto wake atakaowaacha watabarikiwa.
8. Mfalme mwema aketipo kutoa hukumu,huupepeta uovu wote kwa macho yake.
9. Nani athubutuye kusema: “Nimeutakasa moyo wangu;mimi nimetakasika dhambi yangu?”
10. Mizani ya udanganyifu na vipimo vya udanganyifu,vyote ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu.
11. Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake,kama tabia yake ni njema na aminifu.