25. Ni hatari kusema kwa mzaha “Usiahidi kumpa Mungu kitu bila kufikiri,la sivyo utaanza kusikitika baada ya nadhiri yako.”
26. Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu;huwaadhibu bila huruma.
27. Dhamiri ya mtu ni taa ya Mwenyezi-Mungu;huchunguza nafsi yake mtu mpaka ndani kabisa.
28. Wema na uaminifu humkinga mfalme;utawala wake huimarishwa kwa uadilifu.
29. Fahari ya vijana ni nguvu zao,uzuri wa vikongwe ni mvi za uzee.
30. Mapigo yanayoumiza ni dawa ya kuondoa uovu;viboko husafisha nafsi mpaka ndani kabisa.