Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 20:21-30 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Mali iliyopatikana kwa haraka mwanzoni,haitakuwa ya heri mwishoni.

22. Usiseme, “Nitalipiza ubaya niliotendewa.”Mtegemee Mwenyezi-Mungu naye atakusaidia.

23. Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,na vipimo visivyo halali ni kitu kibaya.

24. Hatua za mtu huongozwa na Mwenyezi-Mungu;awezaje binadamu kujua njia ya kwenda?

25. Ni hatari kusema kwa mzaha “Usiahidi kumpa Mungu kitu bila kufikiri,la sivyo utaanza kusikitika baada ya nadhiri yako.”

26. Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu;huwaadhibu bila huruma.

27. Dhamiri ya mtu ni taa ya Mwenyezi-Mungu;huchunguza nafsi yake mtu mpaka ndani kabisa.

28. Wema na uaminifu humkinga mfalme;utawala wake huimarishwa kwa uadilifu.

29. Fahari ya vijana ni nguvu zao,uzuri wa vikongwe ni mvi za uzee.

30. Mapigo yanayoumiza ni dawa ya kuondoa uovu;viboko husafisha nafsi mpaka ndani kabisa.

Kusoma sura kamili Methali 20