1. Divai huleta dhihaka na kileo huleta ugomvi;yeyote anayevutiwa navyo hana hekima.
2. Ghadhabu kali ya mfalme ni kama simba angurumaye;anayemkasirisha anayahatarisha maisha yake.
3. Ni jambo la heshima kuepa ugomvi;wapumbavu ndio wanaogombana.
4. Mvivu halimi wakati wa kulima;wakati wa mavuno atatafuta asipate chochote.
5. Fikira za mtu zimefichika kama kilindi cha maji;lakini mtu mwenye busara ajua kuzichota humo.
6. Watu wengi hujivunia kuwa wema,lakini mwaminifu wa kweli apatikana wapi?
7. Mtu mwadilifu akiishi kwa unyofu;watoto wake atakaowaacha watabarikiwa.
8. Mfalme mwema aketipo kutoa hukumu,huupepeta uovu wote kwa macho yake.
9. Nani athubutuye kusema: “Nimeutakasa moyo wangu;mimi nimetakasika dhambi yangu?”