Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 20:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Divai huleta dhihaka na kileo huleta ugomvi;yeyote anayevutiwa navyo hana hekima.

2. Ghadhabu kali ya mfalme ni kama simba angurumaye;anayemkasirisha anayahatarisha maisha yake.

3. Ni jambo la heshima kuepa ugomvi;wapumbavu ndio wanaogombana.

4. Mvivu halimi wakati wa kulima;wakati wa mavuno atatafuta asipate chochote.

5. Fikira za mtu zimefichika kama kilindi cha maji;lakini mtu mwenye busara ajua kuzichota humo.

6. Watu wengi hujivunia kuwa wema,lakini mwaminifu wa kweli apatikana wapi?

7. Mtu mwadilifu akiishi kwa unyofu;watoto wake atakaowaacha watabarikiwa.

8. Mfalme mwema aketipo kutoa hukumu,huupepeta uovu wote kwa macho yake.

9. Nani athubutuye kusema: “Nimeutakasa moyo wangu;mimi nimetakasika dhambi yangu?”

10. Mizani ya udanganyifu na vipimo vya udanganyifu,vyote ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu.

Kusoma sura kamili Methali 20