Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 2:13-22 Biblia Habari Njema (BHN)

13. watu waziachao njia nyofu,ili kuziendea njia za giza;

14. watu wafurahiao kutenda maovu,na kupendezwa na upotovu wa maovu;

15. watu ambao mienendo yao imepotoka,nazo njia zao haziaminiki.

16. Hekima itakuwezesha kumkwepa mwanamke mwasherati,mwanamke malaya wa maneno matamu;

17. mwanamke amwachaye mwenzi wa ujana wake,na kulisahau agano la Mungu wake.

18. Nyumba yake yaelekea kuzimu,njia zake zinakwenda ahera.

19. Yeyote amwendeaye kamwe harudi,wala hairudii tena njia ya uhai.

20. Kwa hiyo utafuata mfano wa watu wema,na kuzingatia mienendo ya waadilifu.

21. Maana wanyofu wataipata nchi,na waaminifu watadumu ndani yake.

22. Lakini waovu wataondolewa nchini,na wenye hila watangolewa humo.

Kusoma sura kamili Methali 2