Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 2:12-18 Biblia Habari Njema (BHN)

12. vitakuepusha na njia ya uovu,na watu wa maneno mapotovu;

13. watu waziachao njia nyofu,ili kuziendea njia za giza;

14. watu wafurahiao kutenda maovu,na kupendezwa na upotovu wa maovu;

15. watu ambao mienendo yao imepotoka,nazo njia zao haziaminiki.

16. Hekima itakuwezesha kumkwepa mwanamke mwasherati,mwanamke malaya wa maneno matamu;

17. mwanamke amwachaye mwenzi wa ujana wake,na kulisahau agano la Mungu wake.

18. Nyumba yake yaelekea kuzimu,njia zake zinakwenda ahera.

Kusoma sura kamili Methali 2