Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 2:10-19 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Maana hekima itaingia moyoni mwako,na maarifa yataipendeza nafsi yako.

11. Busara itakulinda,ufahamu utakuhifadhi;

12. vitakuepusha na njia ya uovu,na watu wa maneno mapotovu;

13. watu waziachao njia nyofu,ili kuziendea njia za giza;

14. watu wafurahiao kutenda maovu,na kupendezwa na upotovu wa maovu;

15. watu ambao mienendo yao imepotoka,nazo njia zao haziaminiki.

16. Hekima itakuwezesha kumkwepa mwanamke mwasherati,mwanamke malaya wa maneno matamu;

17. mwanamke amwachaye mwenzi wa ujana wake,na kulisahau agano la Mungu wake.

18. Nyumba yake yaelekea kuzimu,njia zake zinakwenda ahera.

19. Yeyote amwendeaye kamwe harudi,wala hairudii tena njia ya uhai.

Kusoma sura kamili Methali 2