10. Maana hekima itaingia moyoni mwako,na maarifa yataipendeza nafsi yako.
11. Busara itakulinda,ufahamu utakuhifadhi;
12. vitakuepusha na njia ya uovu,na watu wa maneno mapotovu;
13. watu waziachao njia nyofu,ili kuziendea njia za giza;
14. watu wafurahiao kutenda maovu,na kupendezwa na upotovu wa maovu;
15. watu ambao mienendo yao imepotoka,nazo njia zao haziaminiki.
16. Hekima itakuwezesha kumkwepa mwanamke mwasherati,mwanamke malaya wa maneno matamu;
17. mwanamke amwachaye mwenzi wa ujana wake,na kulisahau agano la Mungu wake.
18. Nyumba yake yaelekea kuzimu,njia zake zinakwenda ahera.
19. Yeyote amwendeaye kamwe harudi,wala hairudii tena njia ya uhai.