Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 19:5-18 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Shahidi mwongo hataacha kuadhibiwa;asemaye uongo hataepa adhabu.

6. Watu wengi hujipendekeza kwa wakuu;kila mtu hutaka kuwa rafiki ya mtu mkarimu.

7. Maskini huchukiwa na ndugu zake;marafiki zake ndio zaidi: Humkimbia!Hata awabembeleze namna gani hatawapata.

8. Ajipatiaye hekima anaipenda nafsi yake;anayezingatia busara atastawi.

9. Shahidi mwongo hatakosa kuadhibiwa;asemaye uongo ataangamia.

10. Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa,tena ni vibaya zaidi mtumwa kuwatawala wakuu.

11. Mwenye busara hakasiriki upesi;kusamehe makosa ni fahari kwake.

12. Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba,lakini wema wake ni kama umande juu ya majani.

13. Mtoto mpumbavu ni balaa kwa baba yake;na ugomvi wa mke ni kama matone ya mvua yasiyoisha.

14. Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa wazee wake,lakini mke mwenye busara hutoka kwa Mwenyezi-Mungu.

15. Uzembe ni kama usingizi mzito;mtu mvivu atateseka kwa njaa.

16. Anayeshika amri anasalimisha maisha yake;anayepuuza agizo atakufa.

17. Anayemsaidia maskini anamkopesha Mwenyezi-Mungu;Mwenyezi-Mungu atamlipa kwa tendo lake jema.

18. Mrudi mwanao kungali bado na tumaini,lakini usimwadhibu kiasi cha kumwangamiza.

Kusoma sura kamili Methali 19