Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 19:11-24 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Mwenye busara hakasiriki upesi;kusamehe makosa ni fahari kwake.

12. Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba,lakini wema wake ni kama umande juu ya majani.

13. Mtoto mpumbavu ni balaa kwa baba yake;na ugomvi wa mke ni kama matone ya mvua yasiyoisha.

14. Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa wazee wake,lakini mke mwenye busara hutoka kwa Mwenyezi-Mungu.

15. Uzembe ni kama usingizi mzito;mtu mvivu atateseka kwa njaa.

16. Anayeshika amri anasalimisha maisha yake;anayepuuza agizo atakufa.

17. Anayemsaidia maskini anamkopesha Mwenyezi-Mungu;Mwenyezi-Mungu atamlipa kwa tendo lake jema.

18. Mrudi mwanao kungali bado na tumaini,lakini usimwadhibu kiasi cha kumwangamiza.

19. Mtu wa hasira kali lazima apate adhabu;ukimwachia mara moja itakubidi kumwachia tena.

20. Sikiliza shauri na kupokea mafundisho,upate hekima ya kukufaa siku zijazo.

21. Kichwani mwa mtu mna mipango mingi,lakini anachokusudia Mwenyezi-Mungu ndicho kitakachofanyika.

22. Kinachotakiwa kwa mtu ni uaminifu;afadhali mtu maskini kuliko mtu mwongo.

23. Kumcha Mwenyezi-Mungu kunaleta uhai;amchaye hujaliwa pumziko la kutosheleza,wala hatapatwa na baa lolote.

24. Mvivu ni kama mtu atiaye mkono katika sahani ya chakula,lakini hana nguvu ya kuuinua hadi mdomoni.

Kusoma sura kamili Methali 19