Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 19:10-21 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa,tena ni vibaya zaidi mtumwa kuwatawala wakuu.

11. Mwenye busara hakasiriki upesi;kusamehe makosa ni fahari kwake.

12. Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba,lakini wema wake ni kama umande juu ya majani.

13. Mtoto mpumbavu ni balaa kwa baba yake;na ugomvi wa mke ni kama matone ya mvua yasiyoisha.

14. Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa wazee wake,lakini mke mwenye busara hutoka kwa Mwenyezi-Mungu.

15. Uzembe ni kama usingizi mzito;mtu mvivu atateseka kwa njaa.

16. Anayeshika amri anasalimisha maisha yake;anayepuuza agizo atakufa.

17. Anayemsaidia maskini anamkopesha Mwenyezi-Mungu;Mwenyezi-Mungu atamlipa kwa tendo lake jema.

18. Mrudi mwanao kungali bado na tumaini,lakini usimwadhibu kiasi cha kumwangamiza.

19. Mtu wa hasira kali lazima apate adhabu;ukimwachia mara moja itakubidi kumwachia tena.

20. Sikiliza shauri na kupokea mafundisho,upate hekima ya kukufaa siku zijazo.

21. Kichwani mwa mtu mna mipango mingi,lakini anachokusudia Mwenyezi-Mungu ndicho kitakachofanyika.

Kusoma sura kamili Methali 19