Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 19:1-15 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Afadhali maskini aishiye kwa unyofu,kuliko mtu mpotovu wa maneno na mpumbavu.

2. Haifai mtu kuwa bila akili;mwenda harakaharaka hujikwaa.

3. Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake,huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.

4. Mali huvuta marafiki wengi wapya,lakini maskini huachwa bila rafiki.

5. Shahidi mwongo hataacha kuadhibiwa;asemaye uongo hataepa adhabu.

6. Watu wengi hujipendekeza kwa wakuu;kila mtu hutaka kuwa rafiki ya mtu mkarimu.

7. Maskini huchukiwa na ndugu zake;marafiki zake ndio zaidi: Humkimbia!Hata awabembeleze namna gani hatawapata.

8. Ajipatiaye hekima anaipenda nafsi yake;anayezingatia busara atastawi.

9. Shahidi mwongo hatakosa kuadhibiwa;asemaye uongo ataangamia.

10. Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa,tena ni vibaya zaidi mtumwa kuwatawala wakuu.

11. Mwenye busara hakasiriki upesi;kusamehe makosa ni fahari kwake.

12. Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba,lakini wema wake ni kama umande juu ya majani.

13. Mtoto mpumbavu ni balaa kwa baba yake;na ugomvi wa mke ni kama matone ya mvua yasiyoisha.

14. Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa wazee wake,lakini mke mwenye busara hutoka kwa Mwenyezi-Mungu.

15. Uzembe ni kama usingizi mzito;mtu mvivu atateseka kwa njaa.

Kusoma sura kamili Methali 19