Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 18:17-22 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Ajiteteaye kwanza huonekana msema kweli,mpaka hapo mpinzani wake atakapoanza kumhoji.

18. Kura hukomesha ubishi;huamua kati ya wakuu wanaopingana.

19. Ndugu aliyeudhiwa ni mgumu kuliko mji wa ngome;magomvi hubana kama makufuli ya ngome.

20. Maneno ya mtu yaweza kumshibisha;hutosheka kwa matokeo ya maneno yake.

21. Ulimi una nguvu ya kufanya hai na kuua;wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.

22. Anayempata mke amepata bahati njema;hiyo ni fadhili kutoka kwa Mwenyezi-Mungu.

Kusoma sura kamili Methali 18