17. Ajiteteaye kwanza huonekana msema kweli,mpaka hapo mpinzani wake atakapoanza kumhoji.
18. Kura hukomesha ubishi;huamua kati ya wakuu wanaopingana.
19. Ndugu aliyeudhiwa ni mgumu kuliko mji wa ngome;magomvi hubana kama makufuli ya ngome.
20. Maneno ya mtu yaweza kumshibisha;hutosheka kwa matokeo ya maneno yake.
21. Ulimi una nguvu ya kufanya hai na kuua;wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.
22. Anayempata mke amepata bahati njema;hiyo ni fadhili kutoka kwa Mwenyezi-Mungu.