Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 12:6-17 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Maneno ya waovu lengo lake ni kuua,lakini maneno ya waadilifu huwaokoa wanaotishwa.

7. Waovu huangamizwa na kutoweka kabisa,lakini jamaa ya waadilifu hudumishwa.

8. Mtu husifiwa kadiri ya hekima yake,lakini mtu wa fikira mbaya hudharauliwa.

9. Afadhali mtu wa chini anayejitegemea,kuliko ajitakiaye makuu na kukosa chakula.

10. Mtu mwadilifu huwajali wanyama wake,lakini huruma ya mwovu ni ukatili.

11. Mkulima mwenye bidii ana chakula tele,lakini afuataye mambo yasiyofaa hana akili.

12. Waovu hutamani faida isiyo halali,lakini mtu mwadilifu husimama imara.

13. Mtu mwovu hunaswa kwa uongo wake mwenyewe,lakini mwadilifu hutoka katika taabu.

14. Mtu hufanikiwa kutokana na maneno yakekama apatavyo matokeo ya kazi za mikono yake.

15. Mpumbavu huiona njia yake kuwa sawa,lakini mwenye hekima husikiliza shauri.

16. Udhia wa mpumbavu hujulikana mara,lakini mwerevu huyapuuza matukano.

17. Msema kweli hutoa ushahidi wa kweli,lakini shahidi wa uongo hutamka udanganyifu.

Kusoma sura kamili Methali 12