Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 12:4-10 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Mke mwema ni taji ya fahari kwa mumewe;amwaibishaye mumewe ni kama kidonda mifupani mwake.

5. Mawazo ya mwadilifu ni ya haki;mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.

6. Maneno ya waovu lengo lake ni kuua,lakini maneno ya waadilifu huwaokoa wanaotishwa.

7. Waovu huangamizwa na kutoweka kabisa,lakini jamaa ya waadilifu hudumishwa.

8. Mtu husifiwa kadiri ya hekima yake,lakini mtu wa fikira mbaya hudharauliwa.

9. Afadhali mtu wa chini anayejitegemea,kuliko ajitakiaye makuu na kukosa chakula.

10. Mtu mwadilifu huwajali wanyama wake,lakini huruma ya mwovu ni ukatili.

Kusoma sura kamili Methali 12