Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 12:16-28 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Udhia wa mpumbavu hujulikana mara,lakini mwerevu huyapuuza matukano.

17. Msema kweli hutoa ushahidi wa kweli,lakini shahidi wa uongo hutamka udanganyifu.

18. Maneno ya ovyo hujeruhi kama upanga,lakini asemayo mwenye hekima huponesha kidonda.

19. Ukweli hudumu milele,lakini uongo ni wa kitambo tu.

20. Wanaopanga maovu wamejaa udanganyifu moyoni,lakini wanaonuia mema hupata furaha.

21. Waadilifu hawapatwi na jambo lolote baya,lakini waovu wamejaa dhiki.

22. Midomo isemayo uongo ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini watu waaminifu ni furaha yake.

23. Mwenye busara huficha maarifa yake,lakini wapumbavu hutangaza upumbavu wao.

24. Kuwa na bidii kutampa mtu cheo,lakini uvivu utamfanya mtumwa.

25. Wasiwasi moyoni humkosesha mtu raha,lakini neno jema humchangamsha.

26. Mtu mwadilifu huuepa uovu,lakini njia ya waovu huwapotosha wenyewe.

27. Mwindaji mvivu hatapata anachowinda,lakini mwenye bidii atafanikiwa.

28. Uadilifu ni njia ya uhai,lakini uovu huongoza katika mauti.

Kusoma sura kamili Methali 12