10. Mtu mwadilifu huwajali wanyama wake,lakini huruma ya mwovu ni ukatili.
11. Mkulima mwenye bidii ana chakula tele,lakini afuataye mambo yasiyofaa hana akili.
12. Waovu hutamani faida isiyo halali,lakini mtu mwadilifu husimama imara.
13. Mtu mwovu hunaswa kwa uongo wake mwenyewe,lakini mwadilifu hutoka katika taabu.
14. Mtu hufanikiwa kutokana na maneno yakekama apatavyo matokeo ya kazi za mikono yake.
15. Mpumbavu huiona njia yake kuwa sawa,lakini mwenye hekima husikiliza shauri.
16. Udhia wa mpumbavu hujulikana mara,lakini mwerevu huyapuuza matukano.