Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 12:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Apendaye nidhamu hupenda maarifa,bali asiyependa kuonywa ni mjinga.

2. Mtu mwema hufadhiliwa na Mwenyezi-Mungu,lakini mwenye nia mbaya hulaaniwa na Mungu.

3. Mtu hawi imara kwa kutenda maovu,lakini hakuna kiwezacho kumngoa mtu mwadilifu.

4. Mke mwema ni taji ya fahari kwa mumewe;amwaibishaye mumewe ni kama kidonda mifupani mwake.

5. Mawazo ya mwadilifu ni ya haki;mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.

6. Maneno ya waovu lengo lake ni kuua,lakini maneno ya waadilifu huwaokoa wanaotishwa.

7. Waovu huangamizwa na kutoweka kabisa,lakini jamaa ya waadilifu hudumishwa.

8. Mtu husifiwa kadiri ya hekima yake,lakini mtu wa fikira mbaya hudharauliwa.

Kusoma sura kamili Methali 12