1. Apendaye nidhamu hupenda maarifa,bali asiyependa kuonywa ni mjinga.
2. Mtu mwema hufadhiliwa na Mwenyezi-Mungu,lakini mwenye nia mbaya hulaaniwa na Mungu.
3. Mtu hawi imara kwa kutenda maovu,lakini hakuna kiwezacho kumngoa mtu mwadilifu.
4. Mke mwema ni taji ya fahari kwa mumewe;amwaibishaye mumewe ni kama kidonda mifupani mwake.
5. Mawazo ya mwadilifu ni ya haki;mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.
6. Maneno ya waovu lengo lake ni kuua,lakini maneno ya waadilifu huwaokoa wanaotishwa.
7. Waovu huangamizwa na kutoweka kabisa,lakini jamaa ya waadilifu hudumishwa.