Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 12:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Apendaye nidhamu hupenda maarifa,bali asiyependa kuonywa ni mjinga.

2. Mtu mwema hufadhiliwa na Mwenyezi-Mungu,lakini mwenye nia mbaya hulaaniwa na Mungu.

3. Mtu hawi imara kwa kutenda maovu,lakini hakuna kiwezacho kumngoa mtu mwadilifu.

4. Mke mwema ni taji ya fahari kwa mumewe;amwaibishaye mumewe ni kama kidonda mifupani mwake.

5. Mawazo ya mwadilifu ni ya haki;mashauri ya mwovu ni ya udanganyifu.

Kusoma sura kamili Methali 12