Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 10:8-17 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Mwenye hekima moyoni hutii amri,lakini mpumbavu aropokaye ataangamia.

9. Aishiye kwa unyofu huishi salama,apotoshaye maisha yake atagunduliwa.

10. Akonyezaye kwa nia mbaya huzusha taabu,lakini aonyaye kwa ujasiri huleta amani.

11. Kinywa cha mwadilifu ni chemchemi ya uhai,lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na ukatili.

12. Chuki huzusha ugomvi,lakini upendo hufunika makosa yote.

13. Kinywani mwa mwenye ufahamu mna hekima,lakini wasio na akili watachapwa viboko mgongoni.

14. Wenye hekima huhifadhi maarifa,lakini kuropoka kwa mpumbavu huleta maangamizi haraka.

15. Mali ya tajiri ndio ngome yake,umaskini wa maskini humletea maangamizi.

16. Tuzo la mtu mwema ni uhai,lakini mwovu huishia katika dhambi.

17. Anayekubali maonyo anaelekea kwenye uhai,lakini anayekataa kuonywa amepotoka.

Kusoma sura kamili Methali 10