7. Waadilifu hukumbukwa kwa baraka,lakini waovu watasahaulika kabisa.
8. Mwenye hekima moyoni hutii amri,lakini mpumbavu aropokaye ataangamia.
9. Aishiye kwa unyofu huishi salama,apotoshaye maisha yake atagunduliwa.
10. Akonyezaye kwa nia mbaya huzusha taabu,lakini aonyaye kwa ujasiri huleta amani.
11. Kinywa cha mwadilifu ni chemchemi ya uhai,lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na ukatili.
12. Chuki huzusha ugomvi,lakini upendo hufunika makosa yote.
13. Kinywani mwa mwenye ufahamu mna hekima,lakini wasio na akili watachapwa viboko mgongoni.