Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 10:22-27 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Baraka za Mwenyezi-Mungu ndizo ziletazo fanaka,juhudi za mtu haziongezi hapo chochote.

23. Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo;lakini watu wenye busara hufurahia hekima.

24. Anachoogopa mtu mwovu ndicho kitakachompata,lakini anachotamani mwadilifu ndicho atakachopewa.

25. Kimbunga hupita na mwovu hutoweka,lakini mwadilifu huimarishwa milele.

26. Kama ilivyo siki kwa meno au moshi machoni,ndivyo alivyo mvivu kwa bwana wake.

27. Kumcha Mwenyezi-Mungu hurefusha maisha,lakini miaka ya waovu itakuwa mifupi.

Kusoma sura kamili Methali 10