Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 1:14-24 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Njoo ushirikiane nasi,vyote tutakavyopata tutagawana.”

15. Wewe mwanangu usiandamane nao,uzuie mguu wako usifuatane nao.

16. Maana wao wako mbioni kutenda maovu,haraka zao zote ni za kumwaga damu.

17. Mtego utegwao huku ndege anaona,mtego huo wategwa bure.

18. Wao huvizia na kujiangamiza wao wenyewe,hutega mtego wa kujinasa wao wenyewe.

19. Ndivyo zilivyo njia za waishio kwa ukatili;ukatili huyaangamiza maisha ya wakatili.

20. Hekima huita kwa sauti barabarani,hupaza sauti yake sokoni;

21. huita juu ya kuta,hutangaza penye malango ya mji:

22. “Enyi wajinga! Mpaka lini mtapenda kuwa wajinga?Mpaka lini wenye dharau watafurahia dharau zao,na wapumbavu kuchukia maarifa?

23. Sikilizeni maonyo yangu;nitawamiminia mawazo yangu,nitawajulisha maneno yangu.

24. Kwa kuwa nimewaita mkakataa kusikiliza,nimewapungia mkono mje mkakataa,

Kusoma sura kamili Methali 1