Agano la Kale

Agano Jipya

Methali 1:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Hizi ni methali za Solomoni mfalme wa Israeli, mwana wa Daudi.

2. Methali hizi zawapatia watu hekima na nidhamu; zawafanya waelewe maneno ya busara,

3. zawafanya kuwa na nidhamu, utaratibu, uadilifu, haki na kutenda kwa usawa.

4. Huwapatia wajinga werevu na vijana maarifa na hadhari.

5. Mwenye hekima azisikie na kuongeza elimu yake, naye mwenye busara apate mwongozo.

Kusoma sura kamili Methali 1