Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 4:6-10 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Watu wangu wamepata adhabu kubwakuliko watu wa mji wa Sodomamji ambao uliteketezwa ghaflabila kuwa na muda wa kunyosha mkono.

7. Vijana wa Siyoni walikuwa safi kuliko theluji,walikuwa weupe kuliko maziwa.Miili yao ilikuwa myekundu kama matumbawe,uzuri wa viwiliwili vyao kama johari ya rangi ya samawati.

8. Sasa sura zao ni nyeusi kuliko makaa,wanapita barabarani bila kujulikana;ngozi yao imegandamana na mifupa yaoimekauka, imekuwa kama kuni.

9. Afadhali waliouawa kwa upangakuliko waliokufa kwa njaa,ambao walikufa polepolekwa kukosa chakula.

10. Kina mama ambao huwa na huruma kuuwaliwapika watoto wao wenyewe,wakawafanya kuwa chakula chaowakati watu wangu walipoangamizwa.

Kusoma sura kamili Maombolezo 4