Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 4:20-22 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Walimnasa yule ambaye maisha yetu yalimtegemea,yule mfalme aliyewekwa wakfu wa Mwenyezi-Mungu,yule ambaye tulisema: “Chini ya ulinzi waketutaishi miongoni mwa mataifa.”

21. Wakazi wa Edomu, mwaweza kushangilia kwa sasa,mwaweza kwa sasa kufurahi enyi wakazi wa Uzi;lakini kikombe hiki cha adhabu kitawajia pia,nanyi pia mtakinywa na kulewa,hata mtayavua mavazi yenu!

22. Adhabu ya uovu wako ewe Siyoni imekamilika;Mwenyezi-Mungu hatawaacha zaidi uhamishoni.Lakini nyinyi Waedomu atawaadhibu kwa uovu wenu,atazifichua dhambi zenu.

Kusoma sura kamili Maombolezo 4