Agano la Kale

Agano Jipya

Maombolezo 3:9-28 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Njia zangu ameziziba kwa mawe makubwaamevipotosha vichochoro vyangu.

10. Yeye ni kama dubu anayenivizia;ni kama simba aliyejificha.

11. Alinifukuza njiani mwangu,akanilemaza na kuniacha mkiwa.

12. Aliuvuta upinde wake,akanilenga mshale wake.

13. Alinichoma moyoni kwa mishale,kutoka katika podo lake.

14. Nimekuwa kitu cha dhihaka kwa watu wote,mchana kutwa nimekuwa mtu wa kuzomewa.

15. Amenijaza taabu,akanishibisha uchungu.

16. Amenisagisha meno katika mawe,akanifanya nigaegae majivuni.

17. Moyo wangu haujui tena amani,kwangu furaha ni kitu kigeni.

18. Nimewaza “Nimekata tamaa kabisa,tumaini langu kwa Mwenyezi-Mungu limetoweka.”

19. Kukumbuka taabu na kutangatanga kwangukwanipa uchungu kama wa nyongo.

20. Nayafikiria hayo daima,nayo roho yangu imejaa majonzi.

21. Lakini nakumbuka jambo hili moja,nami ninalo tumaini:

22. Kwamba fadhili za Mwenyezi-Mungu hazikomi,huruma zake hazina mwisho.

23. Kila kunapokucha ni mpya kabisa,uaminifu wake ni mkuu mno.

24. Mwenyezi-Mungu ndiye hazina yanguhivyo nitamwekea tumaini langu.

25. Mwenyezi-Mungu ni mwema kwa wanaomtegemea,ni mwema kwa wote wanaomtafuta.

26. Ni vema mtu kungojea kwa saburiukombozi utokao kwa Mwenyezi-Mungu.

27. Ni vema mtu kujifunza uvumilivutangu wakati wa ujana wake.

28. Heri kukaa peke na kimya,mazito yanapompata kutoka kwa Mungu.

Kusoma sura kamili Maombolezo 3